Sunday, March 20, 2016

MUNGU ANAKUPIGANIA KULINGA NA JINSI UNAVYO KIRI.

2 SAMWELI 15:31 -“Mtu mmoja akamwambia Daudi ya kwamba, Ahithofeli yu katika hao waliopatana na Absalomu; Daudi akasema, Ee Bwana, nakusihi, uligeuze shauri la Ahithofeli liwe ubatili.”

Katikati ya vita kubwa au matatizo mengi yana yokukumba kwanza jifunze kukiri  USHINDI tamka NENO zuri katikati ya taarifa mbaya naye MUNGU ataangalia neno lako ili alitimize vile vile kama ulivyolisema.

Daudi aliijua siri hiyo na ndiyo maana alipoletewa taarifa mbaya kuwa Ahithofeli naye amemuasi hapo hapo alimsihi BWANA kugeuza shauri lake na kweli lileshauri baya la Ahithofeli MUNGU alilibadilisha.

2 SAMWELI 17:1-14 -“ …………………..5 Ndipo Absalomu akasema, Basi, mwiteni Hushai, Mwarki, naye, tukasikie atakayosema yeye pia.
 6 Basi Hushai alipofika kwa Absalomu, Absalomu akamwambia, akasema, Ahithofeli amesema hivi; je! Tufanye kama alivyosema? Kama sivyo, sema maneno yako.

 7 Hushai akamwambia Absalomu, Shauri hili alilolitoa Ahithofeli si jema wakati huu.
 8 Hushai akafuliza kusema, Wamjua baba yako na watu wake, ya kuwa ni watu mashujaa hawa, nao wana uchungu katika mioyo yao, kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake nyikani; tena baba yako ni mtu wa vita, hatalala pamoja na watu wake.

 9 Angalia, amefichwa sasa katika shimo, au penginepo; kisha itakuwa, watakapoanguka baadhi yao mwanzo, kila mtu atakayesikia, atasema, Kuna machinjo katika watu wanaofuatana na Absalomu.

 10 Basi hata yeye aliye shujaa, mwenye moyo kama moyo wa simba, atayeyuka kabisa; maana Israeli wote wanajua ya kuwa baba yako ni shujaa, na ya kuwa watu wale walio pamoja naye ni mashujaa.

 11 Kwa hiyo shauri langu ni hili, Waisraeli wote toka Dani mpaka Beer-sheba wakusanyike kwako, kama mchanga wa bahari kwa wingi; na wewe uende vitani mwenyewe.

 12 Hivyo tutamfikia mahali po pote atakapoonekana, na kumwangukia kama vile umande uangukavyo juu ya nchi; wala hatutaacha hata mmoja wao, yeye na watu wote walio pamoja naye.

 13 Tena, ikiwa amejitia katika mji uwao wote, basi Israeli wote wataleta kamba, na kuuendea mji ule, nasi tutaukokota mpaka mtoni, wala halitaonekana huko hata jiwe dogo moja la mawe yake.

 14 Naye Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, Shauri la Hushai, Mwarki, ni jema kuliko shauri la Ahithofeli. Kwa maana Bwana alikuwa amekusudia kulivunja shauri jema la Ahithofeli, ili Bwana alete mabaya juu ya Absalomu.”

Kuna vitu vingi ambavyo BWANA anasubiri neno lako  na usihi wako kwake ili avitimize !.
Jifunze na ujizoeshe kubadilisha taarifa zote mbaya za maisha yako kwa kukiri vizuri kwa kutegea jina la BWANA na utashangaa tuu MUNGU anafanya vile vile kama ulivyosema.

BY PROPHETESS Tumaini

No comments:

Post a Comment