Sunday, March 20, 2016

MUNGU ANAKUPIGANIA KULINGA NA JINSI UNAVYO KIRI.

2 SAMWELI 15:31 -“Mtu mmoja akamwambia Daudi ya kwamba, Ahithofeli yu katika hao waliopatana na Absalomu; Daudi akasema, Ee Bwana, nakusihi, uligeuze shauri la Ahithofeli liwe ubatili.”

Katikati ya vita kubwa au matatizo mengi yana yokukumba kwanza jifunze kukiri  USHINDI tamka NENO zuri katikati ya taarifa mbaya naye MUNGU ataangalia neno lako ili alitimize vile vile kama ulivyolisema.

Daudi aliijua siri hiyo na ndiyo maana alipoletewa taarifa mbaya kuwa Ahithofeli naye amemuasi hapo hapo alimsihi BWANA kugeuza shauri lake na kweli lileshauri baya la Ahithofeli MUNGU alilibadilisha.

2 SAMWELI 17:1-14 -“ …………………..5 Ndipo Absalomu akasema, Basi, mwiteni Hushai, Mwarki, naye, tukasikie atakayosema yeye pia.
 6 Basi Hushai alipofika kwa Absalomu, Absalomu akamwambia, akasema, Ahithofeli amesema hivi; je! Tufanye kama alivyosema? Kama sivyo, sema maneno yako.

 7 Hushai akamwambia Absalomu, Shauri hili alilolitoa Ahithofeli si jema wakati huu.
 8 Hushai akafuliza kusema, Wamjua baba yako na watu wake, ya kuwa ni watu mashujaa hawa, nao wana uchungu katika mioyo yao, kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake nyikani; tena baba yako ni mtu wa vita, hatalala pamoja na watu wake.

 9 Angalia, amefichwa sasa katika shimo, au penginepo; kisha itakuwa, watakapoanguka baadhi yao mwanzo, kila mtu atakayesikia, atasema, Kuna machinjo katika watu wanaofuatana na Absalomu.

 10 Basi hata yeye aliye shujaa, mwenye moyo kama moyo wa simba, atayeyuka kabisa; maana Israeli wote wanajua ya kuwa baba yako ni shujaa, na ya kuwa watu wale walio pamoja naye ni mashujaa.

 11 Kwa hiyo shauri langu ni hili, Waisraeli wote toka Dani mpaka Beer-sheba wakusanyike kwako, kama mchanga wa bahari kwa wingi; na wewe uende vitani mwenyewe.

 12 Hivyo tutamfikia mahali po pote atakapoonekana, na kumwangukia kama vile umande uangukavyo juu ya nchi; wala hatutaacha hata mmoja wao, yeye na watu wote walio pamoja naye.

 13 Tena, ikiwa amejitia katika mji uwao wote, basi Israeli wote wataleta kamba, na kuuendea mji ule, nasi tutaukokota mpaka mtoni, wala halitaonekana huko hata jiwe dogo moja la mawe yake.

 14 Naye Absalomu na watu wote wa Israeli wakasema, Shauri la Hushai, Mwarki, ni jema kuliko shauri la Ahithofeli. Kwa maana Bwana alikuwa amekusudia kulivunja shauri jema la Ahithofeli, ili Bwana alete mabaya juu ya Absalomu.”

Kuna vitu vingi ambavyo BWANA anasubiri neno lako  na usihi wako kwake ili avitimize !.
Jifunze na ujizoeshe kubadilisha taarifa zote mbaya za maisha yako kwa kukiri vizuri kwa kutegea jina la BWANA na utashangaa tuu MUNGU anafanya vile vile kama ulivyosema.

BY PROPHETESS Tumaini

Hukumu ya MUNGU ni tofauti na ya binaadamu.

YOHANA 8:3-11 “Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.
 4 Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.
 5 Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?

 6 Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
 7 Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.

 8 Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.

 10 Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?
 11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.”

Kutoka kwenye huo mstari juu YESU anatuelekezea vitu viwili  navyo ni cha kwanza ni kuwa hakuna mwanadamu mwenye  hadhi/kiwango  cha kuhukumu mweziwe na jambo la pili ahukumuvyo MUNGU ni tofauti na wanadamu.

Ahukumuvyo MUNGU ni tofauti sana na mwanadamu kwa wanadamu waliona sahihi mwanamke huyo kuhukumiwa kwa kumpiga kwa mawe kama ilivyo desturi lakini  kwa upande wa MUNGU haikuwa sahihi kupigwa mawe bali KUSAMEHE.

Yule mchawi ambaye wewe unamuombea afe lakini MUNGU anampa nafasi zaidi kwa kumuhurumia akitegemea yamkini siku moja atatubu ili amuokoe.

Je wewe ni wangapi leo ambao umewahukumu au umeshawanenea mambo mabaya?, Inatakiwa utubu na kumuomba msamaha MUNGU kwa ajili ya wote ambao uliwahukumu kwa kuwa Imeandikwa Luka 6:37 “Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.”

Watu wengine wamekuwa wakihukumu  hata watumishi wa MUNGU pasipo kujua kuwa MUNGU hapendezwi na mtu yeyote kumuhukumu mwenziye na pasipo kujua kuwa hukumu yao sii ya MUNGU na hukumu ya MUNGU ndiyo pekee ya haki.

Hesabu 12:1 Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.
Hapo tunaona miriamu na haruni wakimsema MUsaa na MUNGU hakupendezwa nao hata kidogo.
Wajibu wetu kama wakristo ni kuwaombea yeyote Yule aliye na kosa na sii kumhukumu kwa kuwa lile tulionalo ni kosa kwetu kwa MUNGU linaweza lisiwe kosa..

HESABU 12:7-10 “Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;
 8 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?

 9 Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake.
 10 Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.”

Mungu aliwaadhibu kwa kumsema mtumishi wake.
Yule ambaye wewe unamuhukumu kwamba ni mchafu sana !?,MUNGU hamuhukumu hivyo bali anamhurumia na kumzidishia siku akitegema yamkini siku moja atatubu dhambi zake

Mungu hakati tama na mtu yeyote na hapendi sisi tuhukumu wengine
Sasa nawe badilika na kuwa na mtazamo wa ki MUNGU sahihi kwa kutohukumu yeyote bali kumuhurumia na kumuombea rehema yeyote unayemuhisi anahitaji hukumu.


USIHUKUMU YEYOTE anayekosa BALI funga na kuomba kwa ajili yake na MUNGU atambadilisha na kwa kufanya hivyo MUNGU atapendezwa na wewe sana.

MUNGU anafanya kazi na watu makini/waerevu

ISAYA 1:3 “Ng'ombe amjua bwana wake, Na punda ajua kibanda cha bwana wake; Bali Israeli hajui, watu wangu hawafikiri.”

MUNGU anapendezwa na watu wenye kujituma kufikiri na kuelewa vizuri utendaji wake.
YEREMIA 1:11-12 “Tena neno la Bwana likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi.

 12 Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.”

MUNGU anampima Yeremia kama ana umakini sawa sawa kwa kumuuliza anachokiona !,
Na akagungua kweli anaumakini sawa sawa baada ya Yeremia kujibu kisahihi kile anachokiona.

MUNGU huwa anatupa uwezo mkubwa lakini tatizo huwa ni uvivu,ulegevu,kujisahau,kutojali , wepesi wakukata tamaa nazo huzaa

*Kuchelewa kanisani
*Kujisikia uvivu kuomba na kusoma neno kila siku.
*Kupuuzia ujumbe wa MUNGU na tabia nyingi nyingi mbaya ambazo zina sababisha kupunguza nguvu ya MUNGU ndani yetu.

MUNGU anaweza kuwa amekupa nguvu na ukawa hauitumii ,au amekupa akili na hauitumii kisawa sawa ,sasa ni wakati wa kujitenga na makosa yote na kuamka kutumia kila tulichopewa na MUNGU kwa MAKINI na WEREVU kwa ajili ya utukufu wa MUNGU.

MATHAYO 25:1-12 “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.
 2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.
 3 Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;

 4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.
 5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
 6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.

 7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
 8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.
 9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.

 10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
 11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.
 12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.”

Kutokuwa na Busara ,uhodari ,hekima,maarifa,bidii,umakini na uwerevu kunaweza kukukosesha mbingu hivyo anza leo kuwa navyo hivyo vyote.

Kubali kubadilika pia muombe MUNGU  kila siku na akufanye uwe makini zaidi katika maisha yako.

Thursday, January 21, 2016

UJUMBE MUHIMU KWA WEWE ULIYEPONYWA NA YESU KUPITIA HUDUMA HII.


Kwa kuwa sasa yesu amekuponya.
Jua kuwa:-
i.MUNGU amekuponya ili umfuate yeye kwa kumkubali YESU aweze kukuokoa nawe uwe mwaminifu hata mwisho wa maisha yako naye ndipo atakavyo kuokoa na moto wa milele kama alivyokuokoa katika ugonjwa wako.
Je una mfuataje YESU?.Ni  kwa kutii kila agizo lake unalolisikia kupitia watumishi wake katika huduma hii, kwa kuhudhuria kanisani na katika mafundisho ya vipindi mbali mbali katika kanisa lililo hai.
ii.MUNGU amekuponya ili umtumikie umtumikie kwa njia mbalimbali kama vile:-
a.       Kuchangia gharama mbalimbali za huduma.
b.      Kuwaambia watu wenye shida kama uliyokuwa nayo habari za kuponywa kwako ili nao waje kupokea uponyaji wao kama wewe ulivyopokea uponyaji wako.
c.       Unaweza kumtumikia MUNGU kwa vipawa vyako kama vile uimbaji.
iii.MUNGU amekuponya ili uwe shuhuda kwa watu wengine wanaopitia tatizo kama ulilokuwa nalo.Sasa anza kushuhudia wengi zaidi juu ya kuponywa kwako naye MUNGU atapendezwa zaidi nawe naye atakubariki zaidi na zaidi.
Kwa mawasiliano ya huduma hii piga simu no: 0714 409256 au email:wwc4all@gmail.com
 Au tembelea blog yetu:www.wabarikiwa.blogspot.com, Facebook:WWC MOKOZI

Friday, November 27, 2015

HUDUMA YA KIMUNGU KWA WATU WOTE-WWC

Uponyaji wa kiMUNGU kwa HIV/AIDS, CANCER , matatizo ya uzazi yote na kila aina ya magonjwa.

-Kufungua watu wenye kusumbuliwa na nguvu za giza, mizimu na matego.

-Kurudisha misukule na waliokufa vifo vya kutatanisha.

-Utatuzi  wa matatizo ya mahusiano , Kumrudisha mumeo/mkeo na kuweka kibali cha kipekee katika mahusiano yako/yenu.(Kujenga ndoa halali zilizobomoka).

-Kuweka bahati, mvuto na upendeleo wa KIMUNGU katika biashara.

-Uponyaji wa matatizo ya kutozaa hata kwa wasio na kizazi. Na kadhalika ...

Kupata huduma hizi na zinginezo :tutumie email:wwc4all@gmail.com

Huduma Zote Ni Bure Kabisa
Kupata huduma hizi ni bure kwa kuwa afanyaye kazi hizi si sisi bali ni MUNGU hivyo huduma zote ni bure sisi 
tunatumika tuu kwa neema yake.